
Akizungumza na waandishi Mwenyekiti mtendaji kutoka tay Abdalla
Miraji Othman amesema kituo hicho kinawasaidia vijana katika mambo
mbalimbali ya ujasiriamali na elimu ya ukimwi lakini jambo
lililowavunja moyo nipale vijana wa maeneo hayo kufanya vitendo vya
wizi kwa kuiba TV mbili, Dishi, Friji na mambo mengine.
Hata hivyo amesema lengo la kuanzishwa kituo hicho ni kuwasaidia
vijana wa jimbo la kikwajuni kuweza kupata elimu ya kujiendeleza
lakini lengo hilo bado halijafikiwa kwani mtazamo wao umeenda kinyume
kwa vijana hao na badala yake kituo hicho kinawafaidisha vijana
wengine mbali na kikwajuni.
Aidha mwenyekiti ametoa wito kwa wazazi na walenzi wa jimbo la
kikwajuni kuwanasihi watoto wao kukitumia kituo hicho ili kuweza
kufaidika na elimu zinazotolewa katika kituo hicho.
chanzo: zanzibar24.
Comments