
Wakaazi hao wamesema vijana wengi kutoka maeneo mbalimbali wamekuwa
wakifata chakula kwa mama ntilie hao huku wakaazi hao wakiamini kuwa
sheha wa shehia hiyo ana taarifa kamili za tukio hilo.
Nae sheha wa shehia hiyo hakulizungumzia chochote tatizo hilo huku
akiwatupia lawama wananchi hao kwa kupeleka taarifa kwa vyombo vya
habari badala ya kumpelekea yeye kwa ajili ya kulitafutia ufumbuzi
tatizo hilo.
Hivyo wananchi hao waliiomba Serikali kuliangalia kwa kina tatizo
hilo na kulichukulia hatua kwani linapoteza maadili ya uislam katika
kipindi hichi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.
chanzo:zanzibar24.
Comments