
Akitoa kauli ya serikali mbele ya wajumbe wa baraza la wawakilishi
Balozi Iddi amesema kuibomoa skuli hiyo lengo ni kuwajengea wanafunzi
mazingira mazuri ya kusoma kwani eneo hilo baada ya kukamilika itakuwa
na vurugu litalosababisha wanafunzi kushindwa kusoma na skuli ya
Darajani kuibadilisha ili iyendane na shughuli za kibiashara
zitakazokuwepo darajani.
Hata hivyo amesema dhamira ya serikali ni kujenga mji wa Zanzibar
kuwa katika mazingira bora na wenye kuvutia kimaendeleo ili kukuza
uchumi wan chi.
Kwaupande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa,Serikali
za mitaa na Idara maalumu za SMZ Haji Omar Kheri akijibu hoja za wajumbe
wa baraza la wawakilishi kuwa Serikali imefanya utafiti wa kina na
wataalamu wote wa mji mkongwe,wamipango miji,wamazingira na wamanispaa
na kuamulika kuvunja skuli ya vikokotoni na kupafanya eneo hilo kuwa
shoping moli na mambo yote yamezingatiwa yakiweno ya
kimazingira,kihistoria lengo ni kuleta maendeleo Zanzibar.
chanzo: zanzibar24.
Comments