Serikali: Watu 9 tu ndio wanaostahiki kulipwa fidia Barabara ya Kwerekwe hadi Fuoni.

Serikali imesema itawalipa fidia wananchi wanaostahiki kulipwa kutokana na nyumba zao kuathirika na ujenzi wa barabara ya Mwanakwerekwe hadi Fuoni mara tu taratibu za malipo zitakapo kamilika.

Akijibu swali katika kikao cha Baraza la Wawakilishi Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na usafirishaji, Mhe. Mohammed Ahmada Salum amesema kulingana na muongozo wa mwaka 1983 ni watu tisa tu wanaopaswa kulipwa fidia. 


Na amefahamisha kuwa mwaka hatua hiyo inatokana na 1983 Serikali kuweka michoro maalum kuonesha eneo la hifadhi ya barabara.

Hivyo amesema Serikali haitowalipa wananchi waliojenga kinyume na taratibu na waliopewa hati ya muda kwa makubaliano ya kuendesha shughuli zao za biashara katika maeneo hayo ya Serikali.
chanzo: zanzibar24.

Comments