
Ombi hilo limetolewa na Suleiman Mohd Khalfan ambaye ni mkulima wa zao hilo mbele ya
Mkurugenz muendeshaji wa shirika labiashara ya Taifa Zanzibar ZSTC Dr. Said Seif Said alipokua katika ziara
ya siku moja kisiwani Pemba ya kukagua jinsi hali ya uzaaji wa karafuu ulivyo
na matayarisho ya uvunaji kwa mwaka 2017
na 2018.
Suleiman amesema kutokana na
tamaa iliyojengeka kwa kwa baadhi ya watu juu ya zao hilo kumekua kukijitokeza matendo mbali mbali ya
kihalifu ambayo hufanyiwa wakulima pamoja na wamiliki pindi wanapokwenda kulinda mashamba yao jambo
ambalo limepelekea hufu kubwa juu ya maisha yao.
Amesema hadi kufikia sasa ambapo
tayari karafuu zinaonekana kuanza kuchumwa baadhi ya maeneo ya kisiwa cha Pemba
likini hadi sasa serikali za mitaa
pamoja na vyombo vya ulinzi hawajaweka mikutano na wakulima na kuwaeleza vipi
wamejipa kuwazibiti wazi pamoja na kuwahakikishia usalama wao na mali zao.
Kwa upande wake Mkurugenzi muendeshaji wa shirika hilo Dr. Said Seif
Mzee amesema shirika limejipanga kwa kununua vifaa vyote muhimu kama pishi,majamvi,magunia
na kuwapatia mikopo wakulima ili kuwawezesha kuvuna zao hilo bila ya usumbufu
wa aina yeyote na kwa muda muafaka.
Aidha amesema kuwa wamejipanga kuwasajili wote wanaokodi mashamba ya
serikali,na ya watu binafsi ili
kuhakikisha karafuu zote zinaenda kuuzwa ZSTC na sio pahala pemgine popote.
Dr said amefahamisha kuwa shirika linatarajia kukiboresha zaidi kitengo
cha ulinzi ili kuona hakuna hata tembe moja ya karafuu inasafirishwa magendo.
Mkurugenzi huyo amewataka wananchi wote kuuza karafuu zao ZSTC ili
kuisaidia serikali kupata mapato na kuiwezesha kutoa huduma kwa jamii ambazo ni
muhimu.
Katika ziara hiyo Dr. Saidi alibahatika kutembelea maeneo ya
Mahudusi,Kichunjuu, Mtambile, Mgelema,pamoja na Makuwe katika shamba la
Serikali na kujionea jinsi karafuu zilivozaliwa kwa wingi ambapo ni tofauti na
miaka 10 iliyopita.
Comments