Mnazi Mmoja inakabiliwa na uhaba wa madaktari bigwa wa mifupa.

mnaziWizara ya afya Zanzibar imewataka madereva na wananchi wanaotumia vyombo vya usafiri wa barabara  kuwa makini  pamoja na kuzingatia sheria za barabarani ili kuepusha ajali zinazoweza kuepukika  kwani  Hospitali kuu ya Mnazi mmoja inakabiliwa na uhaba wa madaktari  bingwa katika kitengo cha  mifupa.

Akijibu swali katika kikao cha baraza la wawakilishi Naibu Waziri wa Afya Harusi Said Suleiman amesema kuna  ongezeko kubwa la ajali za barabarani zinazosababisha vifo, ulemavu na hata majeraha makubwa jambo linalohatarisha maisha ya wananchi.


Aidha amesema ongezeko hilo la ajali  linapelekea  kuongezeka kwa mahitaji ya huduma za uchunguzi  na matibabu  ambapo wizara inakabiliwa  na tatizo la uhaba wa madaktari bingwa wa mifupa katika hospitali kuu ya Mnazi mmoja.

Harusi amesema kitengo cha mifupa hivi sasa kinauhaba wa madaktari  bigwa  ambapo kwa sasa kina madaktari wawili, mmoja mzalendo na mwengine  mgeni  nakwamba  wawili wapo masomoni.

Aidha  amesema wizara yake inaendelea  na juhudi za kuhakikisha  kitengo hicho kinapata madaktari na  wahudumu  wenye ujuzi wa kutosha ili kukidhi mahitaji  yaliyopo.
chanzo: zanzibar24.

Comments