Mh. Lowassa: Mzee Ndesamburo alikua shujaa wa kweli wa mabadiliko.

lowassaMh. Edward Lowassa ameeleza kusikitishwa na kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo (Chadema) na kueleza kuwa alikua shujaa wa mabadiliko.

Mzee Ndesamburo amefariki dunia wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Moshi mkoani Kilimanjaro.

Kupitia ukurasa wake wa  twitter  Lowassa ameandika, “Nimesikitishwa sana na kifo cha ghafla cha Mzee Ndesamburo, Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi natoa pole kwa familia na wote. 


Mzee Ndesamburo alikua shujaa wa kweli wa mabadiliko wa miaka mingi na mwenye mchango mkubwa kwenye siasa za demokrasia katika Taifa letu.
chanzo:zanzibar24.

Comments