Balozi Seif amtembelea Mh. Samia ofisini kwake Jijini Dar es salaam.
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Makamo wa pili wa Raisi wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi leo
amemtembelea Makamu wa Rais wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan ofisini kwake.
Viongozi hao wamekuwa na Utamaduni wa kawaida wa kukutana katika
dhana nzima ya mfumo wa kuhudumia Wananchi katika utendaji na
ushirikiano wa pamoja kati ya Serikali zote mbili ile ya Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania na ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Makamu
wa Rais wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia
Suluhu Hassan kulia akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Seif Ali Iddi leo asubuhi Ofisini kwake Jijini Dar es salaam.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akibadilishana mawazo
na Makamu wa Rais wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Jijini Dar es salaam.
Comments