
Hayo aliyasema wakati alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari
huko Uwanja wa Ndege wa Zanzibar mara tu aliporudi katika ziara yake ya
siku tatu nchini Djibouti.
Alisema katika mazungumzo yao na Rais wa Djibouti Ismail Omari
Guelleh ambae alimualika rasmi kutembelea katika nchi yake walikubaliana
kushirikiana katika Mambo saba ya msingi ambayo yatasaidia kuleta
maendeleo ya nchi .
Aidha akiyataja maeneo hayo alisema kuwa watashirikiana katika
kuimarisha ujenzi wa Bandari ,ujenzi wa Miundombinu ya Barabara,
Mawasiliano ya simu na Biashara za viungo (Space) .
Hata hivyo alisema watashirikiana kudhibiti suala zima majangili
wanaohatarisha usafiri wa abiria na mali zao pamoja na kuimarisha ndege
za mizigo ili kuweza kuwapa urahisi wafanyabiasha wa Zanzibar .
Alieleza kuwa katika makubaliano hayo waliweza kukubaliana mambo
mbalimbali ambayo yatailetea ustawi mzuri nchi ya Zanzibar pamoja na
kutengeneza mpango kazi katika nchi zote mbili ilikuweza kufanya
utekelezaji kwenda sambamba .
Dkt Shein alisema kuwa katika ziara yake hiyo ujumbe ambao aliofatana
nao wakiwemo mawaziri waliweza kufanya mazungumzo ya pamoja baina ya
mawaziri wa pande zote mbili na kuweza kukubaliana mambo ya msingi
ambayo waliyowafikiana kuyashungulikia.
Hata hivyo Nchi ya Djibouti waliimba nchi ya Zanzibar kudumisha
mashirikiano ya pamoja kwa viongozi wa ngazi za juu na ngazi za kati
ili waweze kutembeleana na kutaka kupeana msaada wa utaalamu wa suala
zima la utalii kwa upande wa Zanzibar .
Dkt shein alisema alitembelea sehemu ya bandari aliona namna ya
huduma ambazo zinatolewa ni za utaalamu wa kisasa,pia wameweza kuanzisha
shirika la ndege la Djibouti na kuwa na ndege moja kubwa na ndogo ndogo
.
Alifahamisha katika makubaliano yao walikubaliana ndege ya Djibouti
ya mizigo ije Zanzibar ili kuweza kufanya kazi za usafirishaji wa
mizigo katika nchi mbili hizo .
Pia Mhe. Rais alisema katika kuimarisha kampuni ya uvuvi wa
Zanzibar mipango imo katika hatua za mwisho za ukamilishaji na
kunatarajiwa kukodi meli za uvuvi kwa hatua za awali hadi itaponunuliwa
rasmi na meli hizo zitakodiwa kwa bei nafuu na wataalamu ambao
wanatajiwa kulijenga sokojipya la samaki ni Shirika la Misaada ya
Kimataifa la Japani (JICA).
Na Khadija Khamis – Maelezo 10/5/2017 .
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR.
chanzo: zanzibar24.
Comments