Marixie
Mercado, Msemaji wa UNICEF amewaambia waandishi wa habari mjini Geneva
kuwa, kufikia mwishoni mwa mwaka huu, idadi ya watoto wanaokabiliwa na
utapiamlo itaongezeka na kufikia milioni 1.4, kiwango ambacho ni sawa na
ongezeko la asilimia 50 ukilinganisha na mwaka jana 2016.
Amesema
watoto laki mbili na 75 elfu miongoni mwao wapo katika hali mbaya zaidi,
na yumkini wakapoteza maisha karibuni hivi iwapo hatua za dharura
hazitachukuliwa.
Mercado ameongeza kuwa, watoto wenye utapiamlo wa kiwango cha juu
wapo katika hatari ya kupoteza maisha mara tisa kutokana na
kipindupindu, kuharisha na surua.
Somalia ambayo imekuwa kwenye vita vya ndani na hususan mashambulizi
ya kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab kwa zaidi ya miongo
miwili, kwa sasa inasumbuliwa na ukame mkubwa unaoandamana na njaa.
Kwa mujibu wa Mpango wa Chakula Duniani WFP, watu laki mbili na 60
elfu waliaga dunia kutokana na baa la njaa lililosababishwa na ukame
kama wa sasa katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika mwaka 2011, huku nusu
ya vifo hivyo vikiwakabili watoto wadogo wenye umri chini ya miaka
mitano.
chanzo:parstoday.
Comments