Wananchi walalamikia kupanda kwa bei za vyakula katika mwezi huu wa ramadhani.

Wananchi  wamewalalamikia wafanyabiashara wanaouza bidhaa zinazotumika katika mwezi mtukufu wa ramadhani  kuwa hadi sasa wameshindwa  kutekeleza agizo la serikali  kushusha bei kwa bidhaa hizo.
Wakizungumza na  kwa nyakati tofauti  baadhi ya wananchi hao wamesema bidhaa zinazotumika kwa futari bado hazinunuliki ukilinganisha na mwezi wa kula mchana  hali yanayopelekea kushindwa kumudu harama za manunuzi.

Kwa upande wao baadhi ya wafanyabiasha wamekiri kuwa hali ya bei bado ipo juu kutokana na serikali bado haijashusha ushuru licha ya kuwa Rais wa zanzibar Dr.Ali Mohammed Shein kusema serikali itashusha ushuru kwa wafanyabiashara zanzibar ili kuwapa unafuu wanunuzi katika kipindi  hichi cha funga.
Bidhaa zilizolalamikiwa kupanda bei katika kipindi hichi ukilinganisha na awali  kwa upande wa nafaka ni Sukari ambayo kilo 1900 hadi 2000, Tambi kilo  1800,Unga wa sembe kilo 2000 hadi 2200, Njugu mawe kilo 2800 hadi 3000, Choroko kilo 2600 hadi 2800 na kwaupande wa Matunda  nanzi  moja 1500 hadi 2000,Muhogo fungu 2000,Majimbi fungu 5000,Ndizi mbivu dole moja 3000 hadi 5000 chana ya pukusa 3000.
Wakizungumzi hali ya usafi wa soko  wafanyabiashara hao wamesema bado  mazingira ya soko  hayarithishi  licha ya kuchangia  pesa ya ufanyia shughuli hizo kila siku.
chanzo:Zanzibar24

Comments