Wakulima kisiwani Pemba washauriwa kuzitumia mvua zinazo nyesha.

Image result for mkuu wa mkoa wa kaskazini pembaWakulima wa zao la karafuu Wilaya ya Wete Kisiwani Pemba wameombwa kuzitumia vizuri mvua za masika ili kuimarisha kilimo chao.


Akizungumza na wakulima pamoja na wadau mbali mbali wa zao la karafuu wilayani humo katika ukumbi wa zstc  Benjamen Mkapa   Mkuu wa Mkoa wa Kuskazini Pemaba Mh Omara Khamis Othman amesema neema ya mvua ambayo Allah ameetuneemesha nivyema kuweza kuitumikia ipasavyo kwalengo la kujiwekea rasilimali ambazo zitatusaidia hapo baadae.



Amesema wakulima wa zao la karafuu hawana budi kuunga mkono jitihada za Serekali ya Mapinduzi Zanzibara ya kuliboresha zao hilo ikiwa ni pamoja na kuongeza vitalu ili kuondoa usumbufu wa upatikanaji wa miche kwa urahisi zaidi.


Amefahamisha kuwa katika kuthamini jitihada za serekali ipo haja kwa wakulima na wadau wengine kushirikiana kulikuza zao la karafuu ili kurejesha hadhi iliyokuwepo awali isipotee.


Ameeleza kuwa wakulima kwapamoja nihaki yao kuendelea kuwashukuru viongozi wao kuendelea kulinda thamani ya bei ya zao hilo isishuke na kuweza kuleta madhara kwa wananchi pamoja na wadau wengine.


Kupitia mkutano huo maalum Mkuu huyo wa Mkoa amechukua nafasi ya kutoa mkono wa pole kwa wananchi wote waliopata madhara yatokanayo na mvua zinazoendelea kunyesha kuendelea kuwa wastahamilivu  katika kipindi hichi kigumu kwao kwani serekali inaendelea kufanya tathmini juu ya wale wote waliopata majanga hayo na kuendelea kutoa taarifa sehemu husika kadri hali inavyo endelea.

Comments