
Akiwahutubia waumini wa dini ya kiislam katika masjid
L-KHALIL uliopo Mtoni Chake Chake kupitia khutba ya swala ya Ijuma Sheikh Khalfan
Suleiman AL-tiwaniy ambae pia ni mmoja kati ya viongozi wa jumuiya ya Istiqama
Pemba amesema waislam wasikubali kuchezewa na makundi yasiyo watakia mema
katika ibada zao.
Amefahamisha kuwa kila ifikapo mwezi wa Ramadhani huzuka
makundi yanayo sambaza taarifa zisizo sahihi nakuwataka waislam kufuata
mwandamo wa mwezi kulingana na nchi utakako onekana jambo ambalo amesema sio
sahihi.
Ameeleza kuwa makundi ya aina hiyo yanapaswa kujiamulia
wenyewe bila ya kuwashirikisha waumini wengine kwani kufanya hivyo kunaleta mgawanyiko
ndani ya dini ya kiislam.
Aidha amewakumbushia waislam
juu ya muda wakula daku nakusema kuwa muda sahihi wa mwisho ni wakati wa
kupambazuka kwa Alfajiri.
Amefahamisha kuwa waislam wakumbuke mtu kujitoa shahwa
kunasababisha funga yake kupotea hivyo kujiepusha kufanya kitendo hicho
nakutupilia mbali kauli za baadhi ya watu wanao dai kuwa hakubatilisha swaumu
ya mgafungaji.
Sambamba nahayo amewaomba waislam kufunga na kufungua
kulingana na mwendamo wa mwezi na endapo kutajitokeza khitilafu kiongozi mkuu
ambae ni Mufty wa nchi kuweza kuweza kuzungumzia tukio hilo.
Comments