
Akijibu swali katika kikao cha Baraza la wawakilishi huko Chukwani
nje kidogo ya Mjini wa Zanzibar Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mohammed
Ahmada amesema serikali inaelewa tatizo la uhaba wa ardhi na kuanzisha
sheria ya mwaka 2014 ya kuanzisha shirika la nyumba Zanzibar ili liweze
kusimamia ujenzi wa Nyumba za Ghorofa.
Amesema katika kubana matumizi holela ya Ardhi hivi sasa Shirika la
Nyumba linaendelea na mpango wake wa utekelezaji wa Ujenzi wa Nyumba za
ghorofa kwa ajili ya kutowa huduma bora kwa wananchi.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la wawakilishi wameelezea wasiwasi wao
juu ya kuwepo kwa matumizi holela ya ardhi ambapo wananchi wamekuwa
wakijenga nyumba za kuishi bila kufuata sheria na kupelekea kupungua kwa
ardhi katika kuendeleza matumizi mengine ya maendeleo.
chanzo: Zanzibar24.
Comments