
Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter Nape ameandika “Tuliwaahidi na huu ndio mkataba kati ya CCM na Wananchi! Tusipoutekeleza hatutaaminika!”
Tangu alipovuliwa uwaziri, Nape amekuwa akichapisha picha mbalimbali
za shughuli alizokuwa akizifanya nchi nzima kuimarisha chama ili
wananchi waweze kukiamini kabla ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, 2015.
Nape kwa upande wake amekuwa akisema kuwa sasa ni wakati wa
kuwatumikia wananchi wa Mtama walioumuamini na waliokiamini chama chake,
kwani asipofanya hivyo kwa kutekeleza ahadi zake, hatoaminiwa tena.
chanzo:zanzibar24.
Comments