Mambo mawili wasio kubalina nayo ACT katika orodha ya watumishi wa serikali wenye vyeti vya kughushi.

Orodha ambayo ilikua na wafanyakazi wengi kutoka katika hlmashauri na
wachache kutoka katika taasisi nyegine za serikali na mashirika ya
umma.
Chama cha ACT wazalendo kinonesha kuunga mkono kwa uamuzi wa serikali
kuwachukulia hatua watumishi wote wa umma waliobainika kutumia vyeti
feki ikiwemo kuwafukuza kazi na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.
Katika taarifa iliyotolewa na Katibu wa Itikadi, Uenezi na
Mawasiliano wa chama hicho, Ado Shaibu, inabainisha kuwa bila shaka
hatua hiyo itapanda mbegu ya uwajibikaji, kuchochea uadilifu na
kuhakikisha uweledi kwenye utumishi wa umma.
“Mbali na kupongeza, yapo masuala kadhaa yaliyoibuka kwenye uhakiki
huo ambayo tunadhani hayakwenda sawasawa na hivyo basi sisi kwa nafasi
yetu tunao wajibu wa kuyakemea ili kuufanya mchakato huu uende kwa
haki,” alieleza Shaibu.
Katika taarifa iliyotolewa na Katibu wa Itikadi, Uenezi na
Mawasiliano wa chama hicho, Ado Shaibu, inabainisha kuwa bila shaka
hatua hiyo itapanda mbegu ya uwajibikaji, kuchochea uadilifu na
kuhakikisha uweledi kwenye utumishi wa umma.
Aliyataja mambo hayo kuwa ni kitendo cha Rais John Magufuli
kuwasamehe wale watakaojiondosha kazini wenyewe na kuwafikisha kwenye
vyombo vya sheria wale watakaoendelea kubaki kwenye nafasi zao jambo
ambalo ni kinyume cha Sheria na Katiba ya nchi.
Alisema kisheria Rais hana mamlaka ya kumsamehe mtu anayetuhumiwa
kufanya kosa la jinai iwapo mtu huyo hajafikishwa kwenye vyombo vya
sheria na kuhukumiwa. “Madaraka pekee aliyonayo Rais ni kutoa Msamaha
kwa wafungwa wanaotumikia kifungo kama alivyofanya hivi karibuni kwenye
Sherehe za Muungano,” alisema.
Aidha, alitaja jambo jingine ambalo chama hicho hakikuridhika nalo
kuwa ni madai ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki, kuwa mchakato wa uhakiki wa
vyeti haujawagusa wanasiasa na wateule wa rais kwa sababu cheti si sifa
ya kupatikana kwao.
“Ikumbukwe kuwa msingi wa utaratibu huu ni kuhakikisha kuwa taifa
linabaki na watumishi wenye sifa. Waziri Kairuki anasema kuwa sifa pekee
ya Kikatiba ya Viongozi wa kisiasa ni kuwa wajue kusoma na kuandika.
Waziri hakutaka kujiuliza iwapo viongozi wa kisiasa watathibitika
kughushi vyeti ambalo ni kosa la jinai haitawaondolea sifa yao ya
uongozi? alihoji.
Alimshauri waziri huyo mwenye dhamana ya utawala bora
kuona kuwa uhakiki wa vyeti kwa viongozi wa kisiasa na wateule wa rais
kama vile mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya ni muhimu kwa kuwa
unakwenda sambamba na viapo na matakwa ya kimaadili.
Chanzo: HabariLeo na zanzibar24.
Comments