Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira January Makamba amesema atamuandikia barua Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ili apate wataalamu wa miamba kwa ajili ya kutafiti miamba iliyoachia katika milima ya Lushoto.
Akizungumza baada ya kukagua barabara ya Soni –Mombo, Makamba amesema hatari iliyopo ni kuporomoka kwa udogo kutoka kwenye milima, kuachia kwa miamba na kuporomoka kwa mawe makubwa jambo ambalo miaka ya nyuma halikuwepo.
Waziri huyo amesema ili kuepusha maafa yanayoweza kutokea amekusudia kuomba wataalamu kutoka kitengo cha Jiolojia kilichopo chini ya Wizara ya Nishati na Madini ili waende kukagua na kutoa ushauri juu ya kuachia kwa miamba hiyo.
Makamba amesema kuwa kudondoka kwa mawe makubwa kutoka katika milima hiyo kulianza mwaka juzi wakati wa msimu wa mvua.
Comments