
Imedaiwa mahakamani hapo kuwa siku ya tarehe 20/4 2015 huko Kipangani
wete mtuhumiwa huyo alimpiga kwa magongo Hadia Mohd ambae ni mke
mwenziwe na kusababishia maumivu kitendo ambacho ni kosa kisheria.
Mtuhumiwa huyo amba anakabiliwa na mashtaka mawili la mwanzo
lakumpiga mke mwenziwe pamoja na la kuharibu mali aliiomba mahakama impe
dhamana jambo ambalo lilikubali mahakamani hapo na kuachiwa baada ya
kukamilisha masharti ya dhamana.
chanzo: zanzibar24.
Comments