Janga la kipindupindu laikumba Yemen.

Shirika la Afya Dunia limetoa  tahadhari juu ya mlipuko wa kipindupindu kutokana na kunasambaa uginjwa huo kwa  haraka Nchini Yemen siku za karibuni.

Takriban watu 250 wamefariki dunia kwa ugonjwa huo mwezi uliopita na mamia ya watu  wanaripotiwa kuambukizwa kila siku na kwamba mlipuko huo karibuni utakuwa janga kubwa.


Ugonjwa huo ambao unasambaa kupitia uchafu katika chakula na maji, unaweza kudhibitiwa kirahisi, lakini mfumo wa afya nchini Yemen umevurugika kutokana na mapigano yanayoendelea kati ya waasi wa Ki Houthi na majeshi ya serikali, ambayo yanaungwa mkono na muungano wa majeshi yanayoongozwa na Saud Arabia.
chanzo: zanzibar24.

Comments