
Wavuvi hao wakaazi wa Msuka, Wilaya ya Micheweni, Mkoa
wa kaskazini, walikwenda baharini siku ya Jumaapili ya tarehe 21 hadi leo bado
hawajaonekana.
Wavuvi wenyewe ni Khamis hamad Sharif (40), Mbarouk
Said Juma (58), Hamad Abdalla Salim (28), na Ali Abdalla Khamis (52).
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, ndugu wa
karibu wa familia wamesema kuwa, jitihada za makusudi zimekuwa zikifanywa kwa
karibu kwa ushirikiano na viongozi mbali mbali wa Serikali na Wanajamii kwa
kutumia usafiri wa baharini kuwatafuta ndugu zao bila ya mafanikio yoyote hadi
sasa.
Mmoja kati ya Maofisa wa Uvuvi waliofika kijijini hapo
Nd.Hidaya Khamis Hamad, amewataka wanafamilia hao kwa nyakati tofauti kuwa
wastahamilivu katika kipindi hichi na kuendelea na jitihada za kuwatafuta
huku Idara ya Uvuvi nayo ikiwa pamoja nao kwa karibu kwa hali yoyote
itakayotokea.
Comments