Aliyemuua Samira kwa kumtia karoni apandishwa kizimbani.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharib limempandisha kizimba cha mahakama ya Vuga mtuhumiwa Azizi Mbaraka Ali (27) mkaazi wa Meli nne Taveta kwa tuhuma za kutenda  kosa la kuua kwa makusudi.
Imedaiwa mahakamani hapo na muendesha mashtaka Suleiman Maulid mbele ya hakimu Isaya Kayange kuwa mtuhumiwa huyo amedaiwa kufanya kosa hilo tarehe 17/6 2015 huko Kiembe samaki Mkoa wa mjini magharib Unguja ambapo alimuua Samira Sultani Abdallah jambo ambalo ni kosa kisheria.

Mtuhumiwa hakutakliwa kujibu lolote na amepelekwa rumande hadi tarehe 1/6 mwaka huu kesi ya ke itakapotajwa tena.
Itakumbukwa kuwa mifupa ya marehemu huyo ilikuywa ndani ya shimo la karo na wazamia lulu mwezi machi mwaka huu.
chanzo:zanzibar24.

Comments