Wananchi wa Zanzibar watakiwa kuchukua tahadhari katika kipindi hichi cha mvua.

Wananchi wa Zanzibar wametakiwa kuchukua  tahadhari katika kipindi hichi cha mvua zinazoendelea kunyesha kwa kuimarisha mazingira bora katika maeneo yao ili kujikinga na maradhi ya mripuko pamoja na Malaria .

Akizungumza na Zanzibar24 huko ofisini kwake Mwanakwerekwe Afisa Afya Kitengo cha Malaria Khamis Ameir Haji amesema kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha bado hakuna mabadiliko makubwa juu ya maambukizi ya Malaria hivyo jamii inapaswa kuwa na tahadhari ya kina kwa kuimarisha usafi wa mazingira kwa kufukia vidimbwi vya maji machafu na kulima vichaka katika maeneo yao.


Aidha ameyataja maeneo yanayoongoza kuwa na wagonjwa wa malaria Pujini, Majenzi, Kengeja Kisiwani Pemba na kwa upande wa Unguja ni Uzini, Miwani, Donge kipange, Kilimahewa bondeni, Karakana,Kwaalinatu na miembeni.

Ugonjwa wa malaria umepungua hapa Zanzibar chini ya  asilimia moja kutokana na utafiti uliofanywa tokea mwaka 2004 hadi 2006 ukilinganisha na miaka iliyopita ugonjwa huo ulikuwa asilimia 30 hadi 40 .
chanzo:Zanzibar24.

Comments