
Akizungumza na
waandishi wa habari katika maadhisho ya siku ya malaria dunia yalio fanyika
katika ukumbi wa Uwanja wa mpira Gombani Stadiam Chake Chake Pemba amesema ni
haki yakila kiongozi kutoa habari juu ya kile kinacho fanyika ili wananchi waondokane na dhana yakua
serekali waifanyii chochote cha kuwaletea maendeleo ndani ya maeneo yao.
Amefahamisha kuwa
endapo wakuu hao hawatotoa taarifa
kutapelekea kudumaza sekta za serekali nahatimae kushindwa kutekeleza malengo
waliyo yakusudia.
Amesema wakati
umefika kwa viongozi kubalika na kutoa taarifa pale panapo stahiki ili kujenga
imani kwa wananchi juu ya serekali yao.
Katika
maadhimisho haya Bi Mwanajuma amewakumbusha wananchi kuvitumia vyandarua
vinavyotolewa na serekali kwa malengo yaliyo kusudiwa ikiwa ni pamoja
nakujikinga na maradhi ya malaria yanayo
onekana kuwathiri zaidi akina mama na
watoto na sio vinginevyo.
Aidha amesema
kuwa katika kupambana na maradhi hayo jumla ya vyandarua 28689 vimegawanywa
ndani ya wilaya zote za pemba kwa mwaka 2016 ikiwa na lengo la kuwakinga
wananchi na ugonjwa huwo.
Sambamba nahayo
ameeleza kuwa licha ya kutolewa kwa vyandaruwa hivyo serekali imeandaa mkakati
wakupiga dawa majumbani ili kumaliza kabisa ugonjwa huwo amabao umeonekana
kufanikiwa kwa aslimia 99 hapa nchi.
Akichangia katika
mkuna huo mmoja kati ya waandishi hao Hajji Nassor amesama watashindwa kutoa
taarifa kwa wananchi juu ya mambo mbali mbali yanayofanywa na taasisi hizo
kutokana na baadhi ya wizara kutotoa mashirikiano kwa waandishi wa habari
ikiwemo Wiazara ya Afya na Wizara ya Elimu.
Nae Bakar Mussa
kutoka gazeti la zanzibarleo amewaasi wakuu wa taasisi za serekali kuto waona
waandishi wa habari maadui nabadala yake
kuungana kwa pamoja ili kuwaletea wananchi maendeleo.
Comments