Agizo hilo limetolewa kwa nyakati tofauti na Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, wakati akikagua ujenzi
wa barabara za Sakina – Tengeru yenye urefu wa kilometa 14.1 na Southern
bypass yenye urefu wa kilometa 42.5 ambazo kwa pamoja zimegharimu kiasi
cha Sh bilioni 132.3.
Profesa Mbarawa alipotembelea barabara ya kuanzia Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) hadi Mirerani wilayani Simanjiro mkoani
Manyara yenye urefu wa kilometa 27, alisema serikali imetumia fedha zake
za mapato ya ndani kiasi cha Sh bilioni 32.2.
Alisema serikali inatumia gharama kubwa kujenga barabara hizo ili
zisaidie kurahisisha shughuli za kila siku za maendeleo na kuharakisha
kukuza uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla.
Alisisitiza kuwa kila mwananchi anao wajibu wa kuzilinda barabara na madaraja na kuyatunza kwa kujali alama na mipaka yake.
Akizungumza katika Mji wa Mirerani, Profesa Mbarawa alisema pamoja na
eneo hilo kuwa na madini ya vito, lakini tangu dunia iumbwe hawakuwahi
kupata barabara ya lami, lakini Serikali ya Awamu ya Tano imewajengea na
iko karibu kukamilika.
Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Tanroads Mkoa wa Arusha, Mgeni
Mwanga aliwataka wananchi waendelee kuwa wavumilivu wakati miradi hiyo
ikiendelea hasa pale kunapojitokeza changamoto mbalimbali ikiwemo
kuzifunga barabara kwa muda.
chanzo:Habarileo.
Comments