Sera ya nishati ni ya mwaka 2015 na ya gesi ni ya mwaka 2013.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani alibainishwa
malengo ya sera hizo wakati akijibu swali la Mbunge wa Mtwara Mjini,
Maftaha Abdallah Nachuma (CUF).
Mbunge Nachuma alimuuliza Naibu Waziri ni lini serikali itasitisha
usafirishaji wa gesi kutoka mtwara kwenda Kinyerezi ili wana Mtwara
wanufaike na ajira zinazotokana na uchakataji wa gesi hiyo.
Dk Kalemani alisema, kuna miradi miwili inayosafirisha gesi asilia
kutoka Mtwara na Lindi hadi Dar es Salaam, miradi hiyo mipya, mmoja
ulikamilika mwaka 2015 na wa Songas ulikamilika mwaka 2004.
Alisema, gesi inayochakatwa Madimba, Mtwara inasafirishwa kwa bomba
kwenda maeneo mbalimbali nchini kwa matumizi mbalimbali yakiwamo ya
Mtwara, Lindi, Mkuranga na Dar es Salaam.
Dk Kalemani alisema,visima viwili vya gesi katika eneo la Mnazi Bay
vimetengwa rasmi kwa ajili ya kupeleka gesi katika mikoa ya Mtwara na
Lindi.
Pamoja na gesi asilia kutoka mikoa hiyo kutumika kwa kiasi kikubwa
katika uzalishaji takribani asilimia 50 ya umeme unaotumika nchini, gesi
hiyo pia inatumika katika miradi ya kusambaza gesi nyumbani na
viwandani katika mikoa ya Mtwara, Lindi na Dar es Salaam.
Dk Kalemani alisema, Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli
nchini inatekeleza mradi wa kuunganisha gesi hiyo katika Kiwanda cha
Dangote kilichopo Mtwara utakaohitaji takribani futi za ujazo milioni
45.
Pia alisema shirika hilo liko kwenye majadiliano na kiwanda cha
Urenex kinachotarajiwa kujengwa mkoani Lindi ili kiweze kuunganisha gesi
chanzo:Habarileo.
Comments