Inategemea ni upande upi wa mzozo huo mataifa yanaunga mkono.
Mataifa yanayo unga waasi wanaopambana na utawala wa rais wa Syria Bashar al Assad, yameunga mkono shambulio hilo.
Uturuki imepokea vizuri ufyetuaji makombora hayo, wakati afisa wa wizara ya mambo ya nje wa Saudia amemsifu rais Trump kwa ukakamavu wake na Uingereza imejitolea usaidizi kikamilifu.

Kwa upande wake Iran ambayo kama Urusi inaunga mkono serikali ya Syria imeshutumu shambulio hilo.
Moscow imetaja mashambulio hayo kama uchukozi mkali dhidi ya taifa huru. Msemaji wa rais Putin (Dmitry Peskov) amesema kwamba kando na kukiuka sheria za kimataifa , Washington imesababisha uharibifu mkubwa katika uhusiano na Moscow.
Wizara ya mambo ya nje imetangaza kusitishwa kwa makubaliano na jeshi la Marekani yalioundwa kuzuia mashambulio ya angani anga ya Syria.

chanzo:Bbc.
Comments