Rais wa Chama cha madaktari Bingwa wa magonjwa ya wanawake na uzazi Profesa Andrea Pembe alisema mpango kazi huo utaweza kuweka bayana ni wataalam wangapi wanahitajika kwenye upasuaji kuwatosha watanzania wote wenye uhitaji.
Amesema mpango huo pia utaangalia ni vifaa gani vya kisasa vinahitajika sambamba na dawa bora zitakazowezesha kuwatibu wagonjwa kulingana na mazingira yaliyopo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa GE Foundation Asha Varghest alisema lengo la kutengeneza mpango huo ni kuhakikisha mpango huo unazingatia mazingira halisi ya Tanzania na kuweka njia nzuri ya namna utakavyotekelezwa.
chanzo:Mwananchi.
Comments