Mabaraza ya vijana yatakiwa kuunda miradi ya maendeleo.

HABARIViongozi wa Majimbo wametakiwa kutoa ushirikiano  wa dhati kwa mabaraza ya vijana Zanzibar kwa kuwapatia misaada ili wawaeze kubuni miradi ya maendeleo ambayo itayoweza kuwanyanyua na kujiajiri wenyewe.
Akizungumza katika kikao maalum huko Makunduzi kilichoandaliwa na Baraza la Vijana Taifa Katibu wa Baraza la wilaya ya makunduchi Kubwa Haji Tuwani na wajumbe wake  amesema   ili kutimiza azma ya serikali vijana kujiajiri wenyewe hakuna budi kwa viongozi kuwawezesha vijana kwa kuwapa mitaji itayoweza  kuwainua ili  kubuni miradi hiyo.

Kwaupande wake kiongzi wa baraza la Vijana taifa Katibu Mtendaji na Ujumbe wake wamewataka vijana hao kuwacha tabia ya kuwatengemea viongozi wa majimbo na badala yake wabuni miradi ya maendeleo kwani Wizara ya kazi Uwezeshaji ,Wazee,Vijana,Wanawake na Watoto chini ya Idara ya uwezeshaji imekusudia kuwapatia mikopo vijana ili kuendeleza miradi hiyo.
Hata hivyo wametoa wito kwa vijana baada ya kuazisha miradi hiyo  itaweza kuwaingizia Fedha ambazo zitasaidia kuendesha shughuli zao  kufungua Akauni ili kuepusha  migogoro itakayowaondolea uwaminifu kati yao.
Ziara hiyo ya siku moja iliyofanyika katika Wilaya ya kati na kusini unguja ambayo iliyakutanisha mabaraza ya wilaya zote katika mkoa wa kusini.
chanzo:Zanzibar24

Comments