Waziri huyo alionesha kuridhishwa kwake baada ya kufanya ziara mkoani
humo mapema wiki hii kwa lengo la kutathmini utekelezaji unaoendelea
katika kurejea miundombinu ili wananchi waendelee kutumia huduma hizo
kama kawaida.
Katika ziara hiyo, Jenista alitembelea Shule ya Sekondari Nyakato,
Ihumona na Omumwani, Kituo cha Afya cha Kabyaile-Ishezina na Kituo cha
Kulelea Wazee cha Kiilima na kubaini kuwa ujenzi wa kituo kipya cha afya
cha Kabyaile-Ishozi kilichofikia asilimia 80, umetumia takribani kiasi
cha Sh milioni 381.5.
“Nikiri kwamba ukiacha baadhi ya mapungufu kwa watendaji wachache,
wengi mmetupa ushirikiano mzuri kwa kulinganisha hali ilivyokuwa kwa
kuangalia tukio lilivyotokea na hadi hatua za kukabili hatimaye
kurejesha hali,” alisema Jenista, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na
ofisi yake.
Alipongeza jinsi wananchi wa mkoa huo walivyoendelea kushirikiana
katika kutekeleza majukumu hadi kufikia lengo la kurejesha hali ya
kawaida ya mkoa huo katika maeneo yaliyoathirika na tetemeko lililokuwa
na ukubwa wa 5.9 katika vipimo vya Ritcher.
“Kama si ushirikiano wa pamoja kati ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Ofisi ya
Mkoa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania huenda tusingefika
hapa, hivyo tuna kila sababu ya kupongeza juhudi hizi kwa niaba ya
serikali hususani Ofisi ya Waziri Mku, tumefarijika kwa ushirikiano
wenu,”alisisitiza.
Pamoja na pongezi hizo, Waziri alimtaka Katibu Tawala wa Mkoa huo,
Kamishna Diwani Athumani kuendelea kuzingatia taratibu za manunuzi na
kila eneo linalofanyiwa kazi kufuata taratibu, za manunuzi zilizopo
kwani kwa atakayekiuka sheria na taratibu hakutakuwa na msamaha.
chanzo:Habarileo.
Comments