Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa
wakala huo, Emmy Hudson, RITA haijafanya mabadiliko yoyote na kuwa kwa
sasa inafanyia kazi maombi yaliyowasilishwa na chama hicho ya mabadiliko
wa Bodi ya Wadhamini.
“RITA inaufahamisha umma kwamba hakuna mabadiliko yoyote
yaliyoidhinishwa kuhusu Bodi ya Wadhamini ya CUF na maombi
yaliyowasilishwa bado yanafanyiwa kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu
zinavyoelekeza,” alisema Hudson ambaye pia ni Kaimu Kabidhi Wasii Mkuu.
chanzo:Habarileo.
Comments