Mashuhuda katika mkoa huo wa Al Bayda wamesema kuwa, ndege hizo za Marekani zisizo na rubani zimetekeleza hujuma katika maeneo ya kusini na mashariki ya mkoa huo na kusababisha hasara kubwa.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo hujuma hiyo imetekelezwa katika hali ambayo Jumatano usiku ndege kadhaa za Marekani zilionekana zikiruka kwa pamoja katika wilaya ya As Sawma'ah mkoani al Bayda.
Inafaa kuashiria kuwa, Saudia kwa kushirikiana na Marekani, Israel, Uingereza na baadhi ya nchi za Kiarabu, ilianzisha hujuma za kila upande dhidi ya Yemen hapo mwezi Machi mwaka 2015 kwa lengo la kumrejesha madarakani kibaraka wake, Abdrabbuh Mansur Hadi rais wa zamani wa Yemen aliyejiuzulu wadhifa huo na kukimbilia Riyadh.
chanzo:parstoday.
Comments