Muhimbili wahitaji vyumba zaidi vya upasuaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Profesa Lawrence Museru UPUNGUFU wa vyumba vya upasuaji katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam umefanya baadhi ya wagonjwa kusubiri mwaka mzima ili kupata huduma hiyo hali ambayo inaweza kusababisha vifo ama ugonjwa kukua.

Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Profesa Lawrence Museru alisema hayo na kuongeza kuwa, ili kukabiliana na changamoto hiyo, wameanza ukarabati katika majengo yao manne hospitalini hapo likiwemo la akina mama, jengo kuu la upasuaji, watoto na tiba ya meno.


Profesa Museru alisema hospitali hiyo ina vyumba vya upasuaji 13 ambavyo havikidhi mahitaji halisi na utoaji wa huduma bora na za haraka kwa wagonjwa.

Alisema kutokana na upungufu huo, wagonjwa wamekuwa wakisubiri kwa muda mrefu ili kupata huduma ya upasuaji, hivyo Muhimbili imeanza ukarabati wa jengo la upasuaji wa akinamama kutoka vyumba viwili hadi vinne, jengo kuu la upasuaji kutoka vyumba saba hadi nane, jengo la watoto kutoka vyumba viwili hadi vinne na jengo la tiba ya meno kuwa na vyumba viwili.

“Ukarabati huu utasaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa wanaosubiri upasuaji ambapo wengine wamekuwa wakisubiri kwa muda mrefu wakati mwingine kufikia hata mwaka. 

Baada ya ukarabati huu kukamilika, hospitali itaongeza vyumba vya upasuaji saba na kufanya iwe na jumla ya vyumba ishirini,” alisema.
chanzo:Habarileo.

Comments