Waziri wa Habari, utamaduni, sanaa na michezo, Dr. Harisson Mwakyembe
amesema hawezi kuwasilisha taarifa ya upande mmoja na isiyokamilika
kuhusiana na sakata la Mkuu wa mkoa Paul Makonda kuvamia kituo cha
Clouds na kusema kuwa kwake jambo hilo sio kipaumbele katika wizara.
Amesisitiza kuwa yeye kama mwanasheria
ataheshimu kanuni za
asili(Principles of natural justice) kwa kusikiliza upande wa pili wa
tuhuma hizo kisha kuzitolea maamuzi sahihi.
chanzo:zanzibar24.
Comments