Baraza la Habari Tanzania limekemea vikali kitendo cha Mkuu wa mkoa kuvamia kituo cha habari.

Baraza la Habari Tanzania limekemea vikali  kitendo cha  Mkuu wa mkoa wa Dar es salamu Paul Makonda kuvamia kituo cha habari Clous Media akiwa na Askari wakiwa na silaha.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Katibu Mtendaji wa baraza hilo Kajubi Mukajanga amesema kitendo cha kuvamia  chombo cha habari na silaha ni kitendo cha kushtua na kutia hofu waandishi kwani ni kinyume na sheria.

Hata hivyo Kajubi amewataka viongozi wa umma kuyatumia vyema madaraka yao  wakati wa utekelezaji wa majukumu yao  na sio kutumia mabavu kwani kufanya hivo ni kuivunja katiba na kumnyima haki mwandishi katika majukumu ya kazi zake.
Aidha ameviomba vyombo vya sheria pamoja na Mamlaka  husika  kuchukua  hatua za kisheria kutokana na tukio hilo kwani si mara ya kwanza kwa waandishi wa habari kutishiwa maisha  katika kazi zao za uwandishi.
Mapema alitoa wito kwa waandishi kuwa na umoja na ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yao pamoja na kuzingatia maadili ya kazi zao katika uandikaji na utangazaji wa habari  ikiwemo kuepuka kurusha au kuandika habari zisizo na tafiti wa kutosha (balance) ili kuepusha migogoro.
chanzo:Zanzibar24

Comments