Aidha, watu hao wanatuhumiwa kuuza pombe haramu ya gongo, kupatikana
na bangi na walikamatwa katika operesheni inayoendelea katika maeneo
mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Naibu
Kamishna wa Polisi wa Kanda hiyo, Lucas Mkondya alisema watuhumiwa hao
walikamatwa katika operesheni iliyofanyika kuanzia Machi 22 hadi 28,
mwaka huu.
Alisema katika operesheni hiyo walikamata kete 75 za dawa za kulevya,
puli 28, kete 542 na misokoto 103 ya bangi pamoja nalita 93 za pombe
haramu ya gongo.
Aidha, Mkondya alisema watu wawili wanaosadikiwa kuwa ni majambazi
wamejeruhiwa wakati wakirushiana risasi na askari polisi katika eneo la
Magengeni Chamazi.
chanzo:Habarileo.
Comments