Watendaji wa Mikoa na Wilaya pamoja na Makamanda kisiwani Pemba watakiwa kutoa ushirikiano juu ya matuzi mabaya ya mchanga.
Na Asha Salum _ Pemba.
Mh.
Waziri ameyasema hayo wakati akiwasilisha taarifa ya hali halisi ya Rasilimali
ya Mchanga, huko katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo, Weni, Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Mh.Hamadi
amesema kuwa, Serikali imeagiza kwa hatua ya kwanza kupunguza matumizi ya
Rasilimali ya mchanaga kwa kutumia utaratibu nzuri unaokubalika kisheria pamoja
na kutozwa faini kwa wanaokiuka taratibu hizo.
Amesema
kwa kuwa Ardhi ni mali ya Serikali lazima mapato yaonekane kupitia utaratibu wa
tozo zilizowekwa kupitia leseni na vibali vya uchimbaji wa rasilimali hiyo.
Kwa
hatua ya pili Mh.Hamadi amesema kuwa, taaluma inahitajika kupitia ngazi mbali mbali, ili
kuwaelewesha wananchi umuhimu wa kuwepo rasilimali ya Mchanga, matumizi pamoja
na maeneo yalioathirika kutokana na matumizi mabaya yaliopo nchini.
Mkutano
huo wa siku moja ambao ulilenga mkakati madhubuti wa kupunguza kasi ya matumizi
ya Mchanaga uliwashirikisha Makamanda wa Jeshai la Polisi wa Mikoa, Wakuu wa
Mikoa na Wilaya, pamoja na maafisa mbali katika Idara zinzzohusika na Mazingira
Unguja na Pemba.
Comments