WADAU mbali mbali wa Sekta ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Kisiwani Pemba wapendekeza juu ya merekebisho ya sera.
WADAU mbali mbali wa Sekta ya Kilimo, Maliasili,
Mifugo na Uvuvi Kisiwani Pemba, wametoa mapendekezo ya marekebisho ya Sera ya
mwaka 2012 inayotegemewa kufayakazi kwa kutoa miongozo inayokwenda sambamba na
shughuli za kilimo.
Mapendekezo hayo
wameyatoa katika mkutano wa mapitio ya Sera Kilimo, uliofanyika Weni, Wilaya ya
Wete Pemba.
Awali akifungua mkutano
kwa niaba ya Ofisa Mdhamin, Mkuu wa Idara ya Mipango, Sera na Utafiti Pemba,
CHUM HAMAD YUSSUF, amesema marekebisho ya sera hiyo ni kwenda sambamba na
mkakati wa malengo ya mkuza iii kwa kuondoa kasoro zilizopo.
Mkuu huyo wa Idara
alisema kuwa, ni jambo la busara kwa
wadau hao kutoa kasoro na mapendekezo
wanayoona ni muhimu na yamekosekana katika sera hiyo,
ili kufikia malengo
yaliokusudiwa kwa faida ya taifa.
Akiwasilisha sera ya
marekebisho, Afisa Mipango, kutoka Idara ya Mipango Zanzibar, ALI BASHA,
amesema kuwa, marekebisho ya sera hiyo, kwa kiasi kikubwa itasaidia kuondoa matatizo
mbali mbali ya sekta hiyo kiutendaji na kuleta ufanisi wenye tija kwa wakulima.
Mbali na hayo, amesema
kuwa, sera mpya inayofanyiwa mapitio itakuwa na maeneo 23 ambayo yatatilia
mkazo katika maeneo ya kilimo, hasa katika mazao ya mizizi, matunda na mboga
mboga.
Akitoa mapendekezo
katika kuchangia sera hiyo Afisa Kilimo, kutoka Idara ya kilimo Pemba, JUMA
MAALIM FAKI, amesema kuwa, ni vyema sera hiyo ikazingatia vyema mbegu bora
zinazokwenda sambamba na mabadiliko ya tabia ya nchi.
Comments