Dk Kebwe alisema hayo katika hotuba yake ya ufunguzi wa kikao cha
Kamati ya Ushauri ya Mkoa huo (RCC) kilichofanyika jana mkoani humu.
Alisema mkoa wa Morogoro unaungana na Rais kupambana na vita hiyo na
utahakikisha unapambana na wale wote wanaohusika na uzambazaji,
usafirishahi, uuzaji na matumizi ya dawa za kulevya.
Alivitaka vyombo vya dola vya mkoa huo kufuatilia kilimo cha bangi
katika maeneo ya baadhi ya wilaya za mkoa huo na kuhakikisha wale wote
wanaojihusisha wanakamatwa na kupelekwa katika vyombo vya sheria.
Mkuu huyo wa mkoa aliwaagiza wakuu wa wilaya kupitia kamati zao za
ulinzi na usalama kuelekeza nguvu zao kwa kuendesha misako ngazi ya
vijiji na vitongoji kupitia viongozi wa maeneo hayo ili kuwabaini
watumiaji, wasafirishaji na wauzaji wa dawa za kulevya ikiwemo kubaini
mashamba ya bangi.
Dk. Kebwe alisema msako huo unapaswa uwe endelevu na wale
watakaopatikana na makosa hayo wachukuliwe hatua za kisheria kwa
kuwafikisha mahakamani .
chanzo:Habarileo.
Comments