Mshambuliaji wa kujitoa mhanga alijilipua katika katikati mwa waumini katika madhabahu ya Wasufi ya mtakatifu Lal Shahbaz Qalandar katika mji wa Sehwan, mkoa wa Sindh.
Waziri mkuu Nawaz Sharif amelaani shambulio hilo.
Wapiganaji wa Islamic State, Taliban nchini Pakistan na makundi mengine ya wanamgambo, wamekiri kuhusika.
Walioshuhudia wanasema mshambuliaji alijilipua watu walipokuwa wakicheza dansi ya imani.
Vyombo vya habari zinasema alirusha guruneti nakisha akajilipua.
"Niliona miili imetapakaa kote. Niliiona miili ya wanawake na watoto," mwanamume mmoja aliwaambia wanahabari.
chanzo:Bbc.
Comments