Pakistan: Watu 72 wafariki shambulio la Islamic State katika madhabahu.

KarachiWatu 72 wamefariki dunia kwenye shambulio katika madhabahu maarufu ya Wasufi kusini mwa Pakistan, polisi wamesema.
Mshambuliaji wa kujitoa mhanga alijilipua katika katikati mwa waumini katika madhabahu ya Wasufi ya mtakatifu Lal Shahbaz Qalandar katika mji wa Sehwan, mkoa wa Sindh.
Waziri mkuu Nawaz Sharif amelaani shambulio hilo.

Wapiganaji wa Islamic State, Taliban nchini Pakistan na makundi mengine ya wanamgambo, wamekiri kuhusika.
Lal Shahbaz Qalandar, in SehwanMadhabahu hayo ni miongoni mwa yale ya kale zaidi na yanayotukuzwa sana na yalikuwa yamejaa watu Alhamisi, kwani siku hiyo huchukuliwa kuwa tukufu kwa Waislamu kufanya sala katika madhabahu hayo.
Walioshuhudia wanasema mshambuliaji alijilipua watu walipokuwa wakicheza dansi ya imani.
Vyombo vya habari zinasema alirusha guruneti nakisha akajilipua.
16 Feb 2017
"Niliona miili imetapakaa kote. Niliiona miili ya wanawake na watoto," mwanamume mmoja aliwaambia wanahabari.
chanzo:Bbc.

Comments