Mtaka alikuwa anazungumza na gazeti hili, siku moja baada ya
kufanyika kwa Jukwaa la Uchumi mkoani kwake lililoandaliwa na Kampuni ya
Magazeti ya Serikali (TSN) kwa kushirikiana na ofisi yake na pia
kuwashirikisha wadau kadhaa wa maendeleo.
Alisema anajua kuna maeneo Dar es Salaam si rahisi kupata ardhi bure,
lakini Simiyu huu ndio muda wa watu kuchangamkia ardhi kwa ajili ya
uwekezaji na kwamba kinachotakiwa ni uwekezaji huo uwe na faida kwa
jamii, hususani kutoa ajira kwa vijana.
Alisema wamedhamiria kuhakikisha Simiyu inakuwa miongoni mwa mikoa mitano nchini inayoongoza kwa viwanda.
“Tunachoamini ni kwamba haiwezekani kujenga uchumi wa viwanda
Tanzania kama tutaendelea kubaki na Dar es Salaam ileile, Mwanza ileile,
Arusha ileile, Mbeya na Morogoro ileile... Lazima tuongeze mikoa
mingine ya kufanana na hiyo mikoa mikubwa, ili tafsiri ya mwananchi
kuhusu uchumi wa kati ianze kuonekana,” alisema mkuu huyo wa mkoa
kijana.
Wadau wengine waliosaidia kufanikisha jukwaa hilo lililoandaliwa na
TSN, wachapishaji wa magazeti ya serikali ya HabariLeo, SpotiLeo na
Daily News ni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Benki ya NMB, Benki za
TIB Development na TIB Corporate, na Baraza la Taifa la Uwezeshaji
Wananchi Kiuchumi (NEEC).
chanzo:Habarileo.
Comments