Akizungumza katika mkutano huo uliokutanisha asasi mbalimbali Zanzibar mkufunzi wa chuo kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA)Dr.Issa Haji Zidd
amesema bado asasi nyingi zinakabiliwa na matatizo na kurudisha
nyuma malengo kutokana na kukosa msukumo wa pamoja kati ya asasi na
wawekezaji ukosefu wa utaalamu na ushirikiano mdogo kwa wanaasasi.
Mkufunzi huyo amesema asasi za kiraia duniani kote zimekua na
mchango mkubwa katika shughuli mbali mbali za kijamii na serikali hivyo
ni vyema asasi hizo kuthaminiwa.
Amesema katika kuthamini asasi hizo Serikali ya mapinduzi Zanzibar
wameweka utaratibu maalumu wa kuzitambua asasi hizo ikiwa ni pamoja na
kuzipatia usajili rasmi.
Alizikumbusha asasi hizo majukumu yao ni pamoja na kuhakikisha
wanazisaidia jamii katika kukabiliana na changamoto zikiwemo kupambana
na umaskini pamoja na kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake.
Mtoa mada Hassan Jani Masoud amesema licha ya uwepo wa asasi mbali
mbali ambazo zimekuwa na mchango mkubwa kwa serikali bado asasi hizo
zinakabiliwa na matatizo mengi katika utendaji wa kazi zake.
Akitaja miongoni mwa matatizo hayo Hassan amesema mfumo wa kisiasa
Zanzibar unaleta changamoto kubwa kwa asasi za kirai katika kufanya kazi
kutokana kukosa uhuru wa kufanya kazi na kupata ugumu kwenye
kutekeleza majukumu yao.
chanzo:zanzibar24
Comments