Mbunge awataka wanawake kushiriki tendo la ndoa na waume zao.

Katika hali isiyo ya kawaida mbunge mmoja nchini Kenya amewakataza wanawake wa nchi hiyo kukutana kimwili na waume zao ili kuwabana kwenda kujiandikisha katika daftari la uchaguzi mkuu.
Mbunge huyo wa Mombasa, Misho Mboko amesema njia pekee ya kuwabana wanaume kwenda kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa Kenya utakaofanyika mwezi Agosti ni kukataa kushiriki tendo la ndoa hadi wawaonyeshe vitambulisho vya kupigia kura.
“Wanawake hii ni mbinu ambayo mnatakiwa kuitumia, ni njia nzuri. Mkatae kufanya nao mapenzi hadi wawaonyeshe kadi zao za kupigia kura,” alisema Mboko.
Mboko ametumia mbinu hiyo ili wanaume wengi wajitokeze kupiga kura kwa kujiandikisha mapema na kupata vitambulisho kabla ya zoezi la kuandikisha wapiga kura kufungwa Februari, 17.
chanzo;zanzibar24.

Comments