Waziri wa Masuala ya Magharibi, Umoja wa Afrika na Umoja wa Ulaya wa Algeria, Abdul Qadir Masahil amesema mgogoro wa Libya unapaswa kutatuliwa kwa njia ya mazungumzo na kwa kuyashirikisha makundi yote yanayozozana nchini humo. Masahil amesema, makundi ya Libya yanaweza kutatua hitilafu zao na kupata suluhisho la matatizo ya nchi hiyo bila ya uingiliaji wa madola ya kigeni.
Amesisitiza kuwa, changamoto kubwa zaidi ya serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya ni kukabiliana na ugaidi na kwamba serikali hiyo inapaswa kuungwa mkono na nchi zote jirani na jamii ya kimataifa.
Libya ilitumbukia katika vita vya ndani na baadhi ya maeneo ya nchi hiyo yakadhibitiwa na makundi ya kigaidi baada ya kuondolewa madarakani dikteta wa zamani wa nchi hiyo, Kanali Muammar Gaddafi mwaka 2011.
chanzo:parstoday.
Comments