Akikabidhi madastibini hayo yenye thamani ya shilingi milioni 3
katika hospitali ya Mnazi mmoja afisa msaidizi wa masoko na mahusiano wa
(ZSSF) Khatibu Iddi amesema,mfuko huo upo kwa ajili ya kusaidia jamii
hivyo wametoa msaada huo kwa ajili ya kuimarisha mfumo wa usafi na
kuzuia maambukizi kwa watu wanaofika hapo.
Kwa upande wake katibu msaidizi wa hospitali ya mnazi mmoja Abubakar
Khamis Hamad ameipongeza (ZSSF) kwa kutoa msaada huo na kuitaka jamii
kuyatumia madastibini hayo kwa mujibu wa maelekezo na kuwataka kuwa na
mashitikiano ili kutunza mazingira na kuondoa magonjwa ya maambukizi
yanayoweza kujitokeza.
Amesema ” dastibini jekundu ni la taka hatarishi, dastibin la manjano
nilataka za karatisi na dastibini la bluu n la taka za vyakula vyakula”
chanzo;zanzibar24.
Comments