Wananchi wawaibua walioiba dawa hospitali.

Watu wawili akiwemo muuguzi wa Zahanati ya Kijiji cha Kaguruka, wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuiba sehemu ya shehena ya dawa zilizoletwa na Serikali kwa ajili ya wananchi katika Zahanati hiyo.
Wananchi walibaini wizi huo na kuanza kuwashambulia watuhumiwa hao hadi viongozi wa kijiji walipofika na kuwafungia katika ofisi ya kijiji ili kunusuru maisha yao.
Kamanda wa Polisi amesema watuhumiwa hao ambao majina yao yamehifadhiwa waliiba dawa za aina mbalimbali za binadamu na vipimo vya malaria ambavyo thamani yake haijafahamika na kwamba watafikishwa mahakamani.
chanzo; zanzibar24.

Comments