Wananchi watakiwa kupaza sauti zao kupinga Leseni za baa.

Wananchi wametakiwa  kuitumia  fursa yao ya kidemokrasia kujitokeza Mahakamani kupinga  maombi ya wamiliki wa baa ili  wasiweze kupatiwa lessen ya biashara ya vileo kwa baa  zinazoleta usumbufu katika makaazi ya watu.
Akizungumza na Zanzibar24 Kaimu Afisa Sheria Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini B Kinduni Ali Abdalla Haji amesema endapo wananchi watajitokeza  katika uwekaji wa pingamizi kwa baa hizo itaweza kusaidia kuziondosha baa hizo zinazowaletea matatizo na usumbufu.
Hata hivyo amesema licha ya Halmashauri  kutoa elimu katika wadi na shehia za wilaya hiyo juu ya kujitokeza kupinga lakini muamko umekuwa mdogo na hivi sasa imeonekana wananchi wamegoma kupinga baa.
Kwaupande wao baadhi  ya  Wananchi   Wameiyambia Zanzibar24  kuwa hawatojitokeza kupeleka pingamizi zao katika Mahakama ya Vileo kutokana na kuvunjika moyo  kwani   malalamiko yao kutofanyiwa kazi  licha ya kujitokeza kwa wingi kila mwaka.
Jumla ya baa baa 20 zimepeleka maombi ya  kupatiwa lessen kwa mwaka 2017 katika Wilaya ya kaskazini B.
CHANZO; Zanzibar24

Comments