mbele ya maafisa wa baraza la mji wa Chakechake wafanyabiashara hao wamesema kwamba wanaonewa kwa kupandishiwa kodi kila barazala linapojisikia na kubadilishwa kwa mikataba wakiwa katikati ya mwaka.
Hayo yamesemwa leo huko katika ofisi za baraza la mji huo chakechake wakati wakikao cha kupokea taarifa ya mikataba mipya ya mwaka mpya wa 2017, huku wakilalamikia matatizo mbalimbali ikiwemo kutokuwepo huduma kama za maji, sokoni hapo.
Aidha wengine walikwenda mbali zaidi kwa kusema kuwa sasa biashara imeshawashinda na lilobaki nikulichumia baraza pekee jambo ambalo pia hatimae litawashinda.
Akizungumza mbele ya hafla hiyo Mzee Maulid Issa Salum amesema hali ni yakusikitisha kwani hapo awali walikuwa wanalipishwa shilingi elfu 25,000 kwa mwezi kama ada ya kodi lakini sasa wanalipishwa shilingi elfu 50,000 kwa mwezi ambayo ni mara mbili yake na hii amesema ni baada ya baraza kubadilisha makubaliano na kuvigawa vikuta sehemu mbili na kutaka walipwe mara mbili yake.
Amedai baraza kwa sasa halina mashirikiano yeyote na wafanya biashara hao tofauti na hapo awali alipokuwepo mkuregenzi aliyoondoka madarakani bwana Seif Shaaban, kwa kufanya maamuzi peke yao ikiwamo mikataba hiyo na kulitaka baraza liwapunguzie kodi na kuvirudisha vikuta vyao kama awali ili wamudu kufanya biashara.
Nae bw; Juma Salum Abdallah amesema kuwachiwa wafanyabiashara holela mbele ya soko ambao hawakati leseni kunawaumiza mno nakuwarejesha nyuma kwani biashara zao zimekuwa hazitoki na kuwasababishia hasara za maksudi,na kulitakaa baraza liwaondoshe watu hao ili kunusuru biashara zao.
Aidha amesema kauli za “asiyeweza kulipa kodi na aondoke katika kikuta wengine wapo” zinazotolewa na baadhi ya wafanyakazi wa baraza zinawanyong’onyesha na kuzilaani, kwa kusema kuwa huo sio uungwana.
Akijibu masuali hayo Mzee wa baraza bw;Omar Suleiman Omar amesema wakati umebadilika na gharama za maisha zimepanda hivyo wanapaswa kufanya wanayofanya ila ameahidi kushungulikia baadhi ya kadhia ikiwemo kuutambuwa uongozi wa kamati ya wafanyabiashara hao ambao wamelalamika kuwa hata walipoiyunda haikuwa yenye kuzingatiwa.
Mkataba mpya ambao unatoka kila mwaka kwa sasa baada ya miaka miwili kama ilivyokuwa awali unatarajiwa kutolewa siku ya jumaatatu, huku agizo lilipo ni kuwa ukishindwa kulipia ifikapo tarehe 25 ya mwezi utanyanganywa mkataba na kuondoshwa kikutani hapo.
chanzo:zanzibar24.
Comments