Wafanya biashara watakiwa kuchangia wadawati Pemba.

Wafanya biashara wa Chake Chake Kisiwani Pemba wametakiwa kuchangia ununuzi wa madawati ili kuunga mkono juhudi za serekali kutoa elimu bora kwa wanafunzi.

Ushauri huo umetoleawa na Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Salama Mbarouk Khatib wakati akizungumza na wafanya biashara hao huko katika ukimbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba.

Amesema ni jukumu la kila mmoja kuchangia madawati na sikwawafanya biasha pekee bali kila mtu linamgusa kwani wanafunzi wanaopatashida maskulini niwao wenyewe.

"Najua hatuna uwezo wa kununua madawati lakini tukishirikiana kwa pamoja tunaweza kupunguza uhaba huu uliopo kwa sasa"

Ameeleza kuwa ili elimu imfikie mwanafunzi vizuri,  nilazima jukumu la kuhakikisha anapatiwa makazi mazuri yatakayo mjenga katika kujiendeleza kielimu nakuweza kujiandalia mazingira mazuri ya kujisomea.

Amaefahamisha kua katika kuipa msukumo sekta ya elimu wadau mbali mbali wakiwemo wafanyabiashara  pamoja na wengineo kujitolea kwa hiari kuchangia madawani kwani kwa sasa imekua kero kwa skuli nyingi hapa nchini.

 Amesema ili kuondokana na changamoto za madawati katika skuli zetu hapa nchini  nilazima kila mmoja wetu  kuunganisha  nguvu za pamoja kujitolea kwa halia na mali  kwania ya kutokomeza kero hizo zisienee.

"Naaimani sote hatuna uwezo kwani dawati moja linauzwa 350000 lakini tukiwa na nia moja tunaweza"


Kwa upande wao wafanya biashara wa chake chake wamemuhakikishia mkuu huyo wa wilaya  kuwa wapo tayari kuchangia madawati kwa maendeleo ya wanafunzi hususana katika skuli amabazo zinaonaupungufu wa kwani kila mmoja anahaki ya kujisomea akiwa mazingira mazuri.

Comments