Akizungumza na Zanzibar24 nje ya maulidi ya Kumswalima Mtume Muhammad (S.A.W) katika madrasa ya kadiria B huko Bububu Mkuu wa Chuo cha kiislamu Zanzibar Dk.Muhidin Ahmad Khamisi amesema mbali na walimu wa madrasa kujitolea katika kuwasomesha wananfunzi lakini wamekuwa wanakosa malipo maalum kulinganisha na elimu zao.
Hata hivyo ametoa wito kwa wadau wa maendeleo kuwa mstari wa mbele katika kusaidia elimu ya dini ya kiislamu kutokana na baadhi ya madrasa kuwa katika hali isiyoridhisha juu ya kutoa elimu bora kwa wananfunzi.
Akizungumza katika maulidi hayo Mwakilishi wa Jimbo la BUBUBU Masud Abdul Rahman amesema mbali na matitizo yanayowakumba walimu na wananfunzi katika kutafuta elimu ya dini ya Kiislamu laiki pia wanajukumu la kutunza maadili ya kiislamu ili kulinda utamaduni uliopo nchini.
chanzo; Zanzibar24
Comments