Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi katika viunga vya chuo hicho
kilichopo chwaka wilaya ya kati Unguja, wanafunzi hao wamesema kuwa
kitendo cha kuwasimamisha kufanya mitihani kwa madai ya kuvuja bila ya
kuwa na ushahidi si cha kiungwana na kinawanyima fursa za kuonyesha
uwezo wao bila ya kujua hatma yao ya masomo katika siku za baadae.
Aidha wanafunzi hao wamesema kuwa licha ya kuwepo hatua za kudhibiti
mitihani katika Taasisi mbalimbali za Elimu, hatua zinazochukuliwa
zinawagusa wanafunzi kwa kiasi kikubwa huku uongozi na walimu ambao wana
dhamana kubwa ya udhibiti wa mitihani kutochukuliwa hatua yoyote.
Hata hivyo wanafunzi hao wameiomba serikali pamoja na jamiii
kuingilia kati suala hilo ili wapate nafasi ya kuendelea tena na masomo
iwapo wataonekana hawana hatia.
Uongozi wa chuo hicho haukua tayari kuzungumza chochote kuhusu tukio
la kuzuiwa masomo wanafunzi hao na Afisa mmoja wa chuo hicho amedai kuwa
taarifa zinapatikana Chuo kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) Tunguu.
chanzo; zanzibar24.
Comments